UZINDUZI WA USHIRIKIANO KATI YA BODI YA UTALII TANZANIA NA TIMU YA SUNDERLAND YA NCHINI UINGEREZA WAKATI WA MECHI YAO NA TIMU YA CHELSEA

Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imeshirikiana na Timu ya mpira wa miguu ya Sunderland ya Uingereza katika uzinduzi wa utangazaji utalii wa Tanzania pamoja na uhamasishaji wa uwekezaji na maendeleo ya michezo (Destination Partner in Tourism and Sports Development).
Uzinduzi huo ulifanyika tarehe 29 Novemba, 2014 kwenye kiwanja cha “Stadium of Light”, kinachomilikiwa na Sunderland Association Football Club (SAFC)
Tukio hilo lilihudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Balozi Peter Kallaghe, Maafisa waUbalozi wa Tanzania nchini Uingereza, Watanzania waishio nchini Uingereza pamoja na baadhi ya maafisa wa Bodi ya Utalii Tanzania
Wakati wa uzinduzi huokatikakingo zakuta za uwanja yalionekana matangazo
yanayotangaza vivutio vya utalii vya Tanzania ambapokulikuwa na mechi kati ya timu ya Sunderland na Chelsea FC iliyorushwa moja
kwa moja na kituo kinachorusha mechi mbalimbali za mpira wa miguu cha DSTV.
Aidha wachezaji wa timu ya Sunderland walionekana wakiwa wamevaa jezi maalum zilizoandikwa ‘Visit Tanzania’ wakati wakifanya mazoezi kabla ya mechi hiyo.
Bodi yaUtalii Tanzania imetumia fursa yamechi hiyo kuhamasisha wageni mashuhuri kutoka ndani na nje ya Uingereza pamoja na mashabiki wa Timu hizo wa nchi zote duniani kutembelea vivutio vya utalii wa Tanzania
Imetolewa na
BODI YA UTALII TANZANI
01/12/2014


0 comments:

Post a Comment