Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu
alizindua Mkakati wa Utekelezaji wa Jumuiya za Hifadhi ya Wanyamapori
ya Jamii (WMA's) kwenye mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Naura
Springs, Arusha,tarehe 2/7/2015. Mkutano huo ulihudhuriwa na wawakilishi
kutoka Wizara ya Maliasili, Wenyeviti wa Muungano wa Jumuiya za WMAs
zilizoidhinishwa, Wawakilishi wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali ya
USAID,WWF,FZS,AWF, na WCS. Aidha, viongozi wa WMAs, wawakilishi wa sekta
binafsi na Maafisa wanyamapori wa Wilaya pia walihudhuria.
Mhe. Waziri alitoa wito wa kuboresha WMAs nchini na kusisitiza
ushirikiano wa karibu na wizara. Vilevile alisema hadi sasa Tanzania
inajivunia kuwa na WMA 21 zenye ukubwa wa kilometa za mraba 36,237.7
zilizoidhinishwa na kutangazwa katika Gazeti la Serikali. Mhe. Waziri
aliongeza kuwa WMA nyingine 17 ziko katika hatua mbalimbali za
uanzishwaji.
Mhe. Waziri Nyalandu alipongeza waandaaji wa mkutano huo na kusema
kuwa mkutano huu ni wa kwanza kufanyika na kukutanisha Wizara, Jumuiya
zilizoidhinishwa pamoja na wawekezaji wa WMAs .
Mkutano huo ulilenga kubadilishana ujuzi na uzoefu wa utekelezaji wa
shughuli za WMAs; kuwa na uelewa wa pamoja na namna bora ya utekelezaji
wa shughuli za WMAs na kupata mwelekeo wa pamoja wa uendeshaji wa WMA’s





0 comments:
Post a Comment