YAH: KUTANGAZA TAARIFA KWA UMMA JUU YA KUZINGATIA TARATIBU ZA BIASHARA YA MAZAO YA MISITU

Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) inautaarifu umma kwa ujumla hususan wafanyabiashara  na watumiaji  wa mazao ya misitu kuzingatia yaliyomo  kwenye ,Sheria ya Misitu Namba 14 ya mwaka 2002 ambayo pia inatambulika kama Sheria ya Misitu Sura Namba 323 (RE: 2002),  Kanunina Miongozo inayoelekeza taratibu za uvunaji, usafirishaji na jinsi ya kufan ya biashara ya mazao ya misitu.  Sheria na Kanuni inaelekeza yafuatayo:

1.Kila mvunaji wa mazao ya misitu lazima awe na leseni halali ya uvunaji wa mazao ya misitu iliyotolewa na mamlaka husika. Aidha, kila gunia la mkaa lililobebwa na chombo chochote cha usafiri ni lazima liwe limekatiwa risiti halali ya malipo ya serikali;
2. Kila msafirishaji wa mazao ya misitu lazima awe na kibali (Transit Pass -
TP) cha kumruhusu kusafirisha mazao ya misitu ikionyesha mahali mazao hayo yalipotoka na yanapokwenda ikiambatishwa na leseni ya uvunaji;
3.Kila mfanyabiashara lazima awe amesajiliwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kuwa ni mfanyabiasharahalali wa mazao ya misitu;
4.Usafirishaji wa mazao ya misitu ni kuanzia saa 12 asubuhi hadi saa 12 jioni;
5.Ni marufuku kusafiriksha mkaa kwa kutumia pikipiki zinazotumia matairi mawili
6.Bishara ya Mkaa lazima ifanyike katika maeneo maalum yaliyoanishwa katika kila wilaya;
7.Ni marufuku kwa wafanyabiasha ya mkaa kufanya biashara hiyo kandokando ya barabara;
8.Kwa wanunuzi wote wa mkaa kwaajili ya matumizi ya Kaya ni lazima wawe na risiti halali ya serikali inayoonesha malipo yaliyofanyika kwa idadi ya magunia ya mkaa aliyonunua;
Hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa yeyote atakayekiuka utaratibu huu.
Imetolewa na:
Juma S. Mgoo
MTENDAJI MKUU
WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU TANZANIA-D’SALAAM
16 Desemba, 2015


0 comments:

Post a Comment